Majukumu Yetu
  1. Kusambaza huduma ya maji kwa watu kwa mujibu wa sheri ya maji ya Na 5 ya mwaka 2019 na sheria nyingine yoyote inayohusiana na usimamizi wa rasilimalii za maji kwa kuzingatia ubora wa viwango vya maji pamoja na mazingira.
  2. Kusambaza maji kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kutibu maji na kuhakikisha ubora wa maji yanayosambazwa kwa kuzingatia viwango vya ubora vilivyohainishwa kwenye sheria ya maji Na.5 ya mwaka 2019 na kanuni zake.
  3. Kuendeleza na kuitunza miundombinu ya maji.
  4. Kutunza na kulinda vyazo vya maji.
  5. Kupanga na kutekeleza miradi ya maji safi na maji taka.
  6. Kuelemisha na kutoa taarifa kwa umma juu ya afya ya maji, utunzaji wa maji na mambo mengine yanayohusu maji.
  7. Kushirikiana na Serikali za Mitaa juu ya mambo yanayohusu huduma za usambazaji maji na uondoaji wa majitaka.
  8. Kukusanya maduhuri ya maji na ada zote za kisheria zinazotokana na utoaji wa huduma ya maji kwa watumiaji wa huduma.
  9. Kupendekeza viwango vipya vya bei za maji.