Chanzo cha Maji cha Mwena ni chanzo cha chemchemi kilichopo kwenye safu ya milima ya Makonde ambacho kina uwezo wa kuzalisha lita 720,000 kwa siku, na kwa sasa uzalishaji halisi ni lita 433,000 kwa siku. Chanzo hiki kinahudumia baadhi ya vijiji vilivyo kando ya bomba kuu linalokwenda Mji wa Masasi ambavyo ni;Chikundi,Mbaju,Chigugu,Mandiwa, Chikukwe,Liloya,Namakongwa, Mailisita,Magumchila na Chisegu.Wanainchi wa maeneo tajwa wanapata huduma ya majisafi na salama kutoka katika chanzo cha chemichemi za Mwena.

