Wajibu wa Mteja

Wateja wanazohaki mbalimbali zilizoanishwa na pia wanawajibika kwa Mamlaka katika kutekeleza mambo mbalimbali kama yalivyoainshwa hapo chini.

 

  1. Kulipa ankara za maji kwa wakati.
  2. Kutoa ushirikiano kwa watumishi wanaowahudumia
  3. Kutoshawishi watumishi ili mteja ahudumiwe kwa upendeleo.
  4. Kuhudhuria mikutano au miadi kwa wakati uliopangwa.
  5. Kutoa taarifa sahihi zinazotakiwa kwa usahihi na kwa wakati unaotakiwa.
  6. Kuzingatia taratibu za kisheria kwa huduma zozote wanazostahili kupatiwa.
  7. Kufuatilia Ankara yake ya mwezi endapo hatapata .
  8. Kuwapokea wafanyakazi kwa heshima na unyenyekevu.
  9. Kutoa kwa wakati taarifa kamili na sahihi kwa kuzingatia aina ya huduma wanayohitaji kutoka Mamlaka.
  10. Kuheshimu amri na maelekezo ya MANAWASA na Mamlaka nyingine za usimamizi na udhibiti wa huduma za maji.
  11. Kutoa mrejesho juu ya huduma za Mamlaka pale ambapo matarajio yanakuwa hayajakidhiwa kwa muda mwafaka bila uoga wala kisasi.
  12. Kuhakikisha miundombinu ya maji kwenye eneo lako na hata maeneo mengine hayavuji.
  13. Kutoa taarifa kwa Mamlaka juu ya vitendo vyovyote vinavyohatarisha usafi na usalama wa maji.
  14. Kuzuia wizi, uharibifu na michepusho ya mita.
  15. Kutoa taarifa kwa Mamlaka juu ya mtumishi yeyote anayeendekeza vitendo vya rushwa.
  16. Mteja atawajibika na ulinzi wa dira ya maji iliyowekwa katika eneo lake, na endapo utatokea uharibifu wowote wa dira atagharamia mwenyewe.
  17. Mteja atawajibika kununua vifaa vya matengenezo ya bomba linalomuhudumia endapo utatokea uharibifu wowote ule.
  18. Kutoa ushirikiano kwa watumishi wa Mamlaka wanaowahudumia.
  19. Kutoa maoni kuhusu mipango na huduma zitolewazo na Mamlaka.
  20. Kutoharibu miundombinu ya majisafi na usafi wa mazingira.
  21. Kutoa taarifa kuhusu uharibifu wa miundombinu na vyanzo vya maji.
  22. Kutoa taarifa kuhusu uvujaji wa maji.